Header Ads

Taarifa muhimu kutoka baraza la Mitihani Tanzania katika viwango vya ufaulu....

VIWANGO VYA UFAULU (GRADE RANGES) ZA MITIHANI HAZIJABADILIKA

Baraza la Mitihani la Tanzania limekuwa likipigiwa simu na watu mbalimbali wakiomba ufafanuzi kuhusu taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa limebadilisha Viwango vya Ufaulu (Grade Ranges).

Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwajulisha watahiniwa na umma kwa ujumla kuwa taarifa hizo ni za UONGO na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki.

Hivyo, Baraza linaomba umma kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa Baraza halijafanya mabadiliko yoyote kuhusu Viwango vya Ufaulu vinavyotumika sasa.


Imetolewa na,

AFISA HABARI NA UHUSIANO

No comments

Powered by Blogger.