Aya ndo mambo ya Dr. Magufuli
Mteule wa kuwania urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu ujao, John Pombe Magufuli na Katibu Mwenezi wa CCM, Nape NNauye wakipiga ngoma.
WAKATI mteule wa Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu ujao, John Pombe Magufuli akifahamika kama mtu makini kwenye utekelezaji wa majukumu yake, imethibitika kuwa waziri huyo wa Ujenzi pia ni mkali kwenye upigaji wa tumba, Risasi Jumamosi linakupa zaidi.
Mathalan, katika uzinduzi wa daraja la Mbutu, wilayani Nzega mkoa wa Tabora, uliofanyika Januari 7, 2013, Magufuli alionekana akipiga Tumba wakati bendi kongwe ya Msondo Ngoma ikitoa burudani katika hafla hiyo, akiwa sambamba na wanamuziki wa kundi hilo, Shaaban Dede na Hassan Moshi ‘TX Jr.
Aidha, wabunge wawili wa upinzani, John Mnyika (Ubungo) na Halima Mdee wa Kawe, watakuwa ni mashuhuda wa uhodari wa Magufuli, kwani katika hafla ya uzinduzi wa barabara ya Msewe- Baruti iliyofanyika miezi michache iliyopita, mteuliwa huyo wa CCM aliifanya tena shughuli hiyo mbele ya umati wa wananchi waliohudhuria.
No comments